DRC: AU yatoa wito wa usitishaji mapigano, huku M23 wakitoa muda wa saa 48 kwa jeshi kuweka silaha chini

DRC: AU yatoa wito wa usitishaji mapigano, huku M23 wakitoa muda wa saa 48 kwa jeshi kuweka silaha chini

Mwenyekiti wa Tume ya Muungano wa Afrika Moussa Faki Mohammat amezitaka pande husika na mzozo wa mashariki mwa jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuheshimu mikataba ya usitishaji mapigano na kumaliza uhasama baina yao.

Haya yanajiri huku huku M23 wanaopigana na jeshi la DRC kwa la kuuteka mji wa Goma wakitoa muda wa saa 48 kwa jeshi kuweka silaha chini.

Moussa Faki Mohammat amesema ametambua kuzorota kwa hali ya usalama na ya kibinadamu Mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Katika taarifa yake kuhusu mzozo huo mkuu huyo wa AU amesema anahofia kuwa hali inayoendelea mashariki inatishia juhudi kubwa zilizofanyika za kurejesha amani, husan mchakato wa upatanishi uliosimamiwa na Rais wa Angola Joao Lourenço.

Bw Mohammat amesisitiza kuwa anaunga mkono juhudi za aina hiyo ambazo amesema ndio njia pekee yakukomesha uhasama baina ya DRC na Rwanda na DRC na wapiganaji wa M23.

Katika taarifa yao M23 – wapiganaji wanaodaiwa kuungwa mkono na Rwanda na ambao wameyateka maeneo ya Kivu Kusini na Kaskazini wanalaani ‘’vitendo vya hivi karibuni vya kigaidi vinavyofanywa dhidi ya raia wa Congo, hasa wakazi wa Goma’’.

‘’Tunatoa wito kwa taasisi, mashirika na mashirika yote yanayohusika na utoaji wa huduma ya maji na umeme jijini humo kuchukua hatua za haraka ili kurejesha huduma za msingi za kijamii kwa manufaa ya wananchi’’.

AFC/M23 inatoa wito kwa wanajeshi na washirika wote wa Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (FARDC) waliopo Goma na viunga vyake kuweka chini silaha zao ndani ya saa 48.

‘’Pia tunatoa wito kwa MONUSCO kusitisha mara moja ushirikiano wake na vikosi vya FARDC na genocidal ambavyo vinarusha mabomu katika maeneo yenye watu wengi na kushambulia maeneo yetu’’, imeeleza taarifa hiyo.

Ufitinema Aime Gerard

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *